Monday, May 3, 2021

Kanisa la PBIM chini ya Prophet Bruno Massae wawakumbuka Yatima, Wajane

 

Kanisa la Prophetic & Biblical International Ministry (PBIM) Iringa limetoa msaada wa chakula na vifaa vya shule wajane na watoto yatima zaidi ya 200 kupitia ibada maalum iliyofanyika kanisani hapo.

Pia, walikabidhi msaada huo kwenye Shule ya Watoto wasiosikia ya Mtwivila, Manispaa ya Iringa.

Nabii wa kanisa hilo, Bruno Massae amesema lengo la msaada huo ni kupanda mbegu ya upenzi kwa jamii ambayo inapaswa kuwajali na kuwasaidia wahitaji kama wajane na watoto yatima.

Akizungumza kwenye ibada hiyo, Diwani wa Kata ya Mkimbizi, Eliud Mvela amelipongeza kanisa hilo kwa utaratibu wake wa kuisaidia jamii ya watu wasiojiweza kila mwaka.

“Niombe taasisi nyingine kwenye kata hii kuiga huu mfano, tuwasaidie wahitaji na huo ndio upendo,” amesema Mvella.




Diwani wa kata ya Mbimbizi, Eliud Mvella ambaye alikuwa mgeni rasmi



Prophet Bruno Massae akihubiri kanisani hapo

Thursday, January 14, 2021

IBRAHIM NGWADA - "TUTASIKILIZA KERO ZA ARDHI KILA ALHAMSI YA MWISHO WA MWEZI


 Meya wa Manispaa ya Iringa, Ibrahim Ngwada ameamua kutenga siku moja kila mwezi ka ajili ya kusikiliza kero za wananchi, kuhusu migogoro ya ardhi.

Amesema kila Alhamisi ya mwisho wa mwezi itakuwa muafaka kwake akishirikiana na wataalamu wa ardhi kuketi na kuwasikiliza wananchi wa Manispaa ya Iringa.

Ngwada alikuwa akizungumza leo katika kikao cha mabalozi wa nyumba kumi ambacho Waziri Mkuu Mstaafu na Mezi wa CCM Mkoa wa Iringa, Mizengo Pinda.

Amesema migogoro ya ardhi ni kati ya kero alizokutana tangu aapishwe kuwa Meya wa Manispaa ya Iringa.

Kero nyingine za wananchi alizoahidi kupambana nazo ni tabia ya baadhi wa watendaji wa mitaa na kata kutaka rushwa wanapotakiwa kutoa barua za dhamana.

Mh Ngwada amesema wamepania kubuni vyanzo vingi vya mapato ili kukuza uchumi wa manispaa na kuondoa tozo ndogo dogo zinazowamiza wananchi.

“Tumekubaliana kushirikiana kwa kiasi kikubwa mimi na Mbunge, Mh Jesca Msambatavangu na tumejipanga kuhakikisha kunakuwa na mabadiliko,” amesema.



Sunday, October 25, 2020

DAUD YASIN, MWENYEKITI WA CCM MUFINDI AOMBA KURA ZA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI KWA UNYENYEKEVU


Kwa unyenyekevu mkubwa naomba kura yako trh 28 kwa Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli. Wagombea Ubunge wote wa CCM na  Wagombea Udiwani 

Daud Yassin 

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi

Saturday, December 14, 2019

Master King anakukaribisha kwenye kongamano la maombi Disemba 22, Sama Hall Tabata Kimanga

Nabii kutoka Kanisa la El Giobboh, Paul John *Master King Paul* anakukaribisha kwenye kongamano la maombi na Maombezi litakalo fanyika Disemba 20 mpaka 22.

Kongamano hilo litafanyika Tabata Kimanga kwenye kwenye ukumbi wa Sama Hall.

Njoo ukutane na Mungu atakaye kuonyesha mambo makubwa na magumu usiyo yajua.

Waimbaji mbalimbali watakuwepo kwenye kongamano hilo.
Jane Misso, Dk Tumaini Msowoya, Mariam Kilyenyi, Elizabeth, Samwel Deo na Theresia.

Usipange kabisa kukosa..

Friday, August 23, 2019

MARIAM KILYENYI AWASHA MOTO TENA DAR

Kwa mara nyingine, mwimbaji wa nyimbo za Injili anayetikisa nchini Mariam Kilyenyi anatarajia kuachia albamu yake ya video inayoitwa Hakimu wa Haki katika uzinduzi utakaopambwa na waimbaji lukuki.

Uzinduzi huo unatarajia kufanyika Jumapili ya Septemba 29, 2019 kwanzia saa saba mchana katika kanisa la uamsho Pentecoste church kwa mchungaji Lilian Kadodo, Ubungo Shekilango.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mariam aliwataja baadhi ya waimbaji watakaomsindikiza kuwa ni DR Tumaini Msowoya Bahati Bukuku,Madame Ruth, Edson Mwasabwite Joyce Ombeni, Robert mwanja, Sarah Mghamba, Loyce Nducha Tumaini Njole, Stephania Masawe na Eddah Mwampagama.

Wengine ni Agnes Nkungwe, Elizabeth  Shimanje,Jamuhury Zacharia, Tumaini Mwasubila, Hafsa kazinja,Magreth Sembuche Kisa ludutu  Glory Moses ,Biver Kasigala, Surprise France silvia Alexander ,Neema Mahhu,Bella kombo na Pst Grace Rendi

Aliwataja wengine kuwa ni w  Dk Donald Kisanga, Stellah Joel,Alfonce Mutema, Daudi Nyigo, Yasinta Kadawele huku mwimbaji Jack Mgaza kutoka South Africa akiwa  mmoja kati ya wageni maalum walioalikwa sambamba kabsaaaa na Agnese bilama kutokea Arusha.

Saturday, April 27, 2019

NAIBU SPIKA-DR TULIA AKSON MGENI RASMI MKESHA WA WAIMBAJI MKOA WA MBEYA

Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Tulia Akson anatarajia kuwa mgeni rasmi katika mkesha wa Umoja wa waimbaji wa muziki wa Injili katika Mkoa wa Mbeya.

Mkesha huo unatarajia kufanyika Mei 3, 2019.

Mwenyekiti wa Umoja huo, Tumaini Mbembela amesema mwimbaji mkongwe Mchungaji Happy Kamili na John Mwakatenya ndio watakao hubiri siku hizo katika kanisa la Mchungaji Mwafongo.

Akizungumza na Gospo Yetu Tanzania, Mbembela amewasihi waimbaji wa mkoa wa Mbeya na wakazi wote kwa ujumla wasipange kukosa mkesha huo kwa sababu pamoja na mambo yote watapata nafasi ya kuzungumza na Mungu.



Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa yenye waimbaji wa nyimbo za Injili wenye umoja wa nguvu unaowasaidia katika kuipeleka kazi ya Mungu mbele.
"Karibuni sana kwenye mkesha hakika tutamuona Mungu.

UMOJA WA WAIMBAJI WA GOSPO MBEYA KUFANYA MKESHA MKUBWA MEI 3,2019

Umoja wa waimbaji wa muziki wa Injili katika Mkoa wa Mbeya unatarajia kufanya mkesha mkubwa wa maombi, kusifu mkoani humo Mei 3, 2019.

Mwenyekiti wa Umoja huo, Tumaini Mbembela amesema mwimbaji mkongwe Mchungaji Happy Kamili na John Mwakatenya ndio watakao hubiri siku hizo katika kanisa la Mchungaji Mwafongo.

Akizungumza na Gospo Yetu Tanzania, Mbembela amewasihi waimbaji wa mkoa wa Mbeya na wakazi wote kwa ujumla wasipange kukosa mkesha huo kwa sababu pamoja na mambo yote watapata nafasi ya kuzungumza na Mungu.



Mkoa wa Mbeya ni kati ya mikoa yenye waimbaji wa nyimbo za Injili wenye umoja wa nguvu unaowasaidia katika kuipeleka kazi ya Mungu mbele.
"Karibuni sana kwenye mkesha hakika tutamuona Mungu.

Kanisa la PBIM chini ya Prophet Bruno Massae wawakumbuka Yatima, Wajane

  Kanisa la Prophetic & Biblical International Ministry (PBIM) Iringa limetoa msaada wa chakula na vifaa vya shule wajane na watoto yati...